Header Ads

ad

Breaking News

Balotelli amzadiwa mabao mama mlezi


Balotelli

WARSAW, Poland
MARIO Balotelli, amesema kiwango alichokionesha na kuiwezesha timu yake ya Italia kushinda mabao 2-1, dhidi ya Ujerumani katika hatua ya nusu fainali ya mataifa ya Ulaya, ni usiku bora katika maisha.

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 21, anayeichezea timu ya Manchester City, alifunga mabao mawili katika kipindi cha kwanza na kuiwezesha Italia kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, mabao hayo ametoa zawadi kwa mama yake mlezi, Silvia. 

"Balotelli alifanya kila awezalo kwa England, lakini alipata zawadi yake dhidi ya Ujerumani. Kiwango chake kilikuwa cha hali ya juu. Kilikuwa cha juu, nguvu na kufanikiwa kupata mabao. Aliongeza kila kitu tulichokitaka kuongezwa kwenye mchezo. Kilikuwa kiwango kizuri." 

Azzurri, sasa itaumana na Hispania katika mechi ya fainali ya michuano hiyo.  
"Ulikuwa usiku wenye furaha katika maisha yangu ninaamini Jumapili utakuwa zaidi," alisema Balotelli.
Balotelli, aliiangailia familia yake akiwakumbuatia. "Mwisho wa mchezo, nilirejea kwa mama,  kwamba ilikuwa wakati mzuri," aliongeza. 

"INilimwambia mama kuwa, mabao niliyofunga ni wa ajili yako. Nilikuwa nikiisubiri siku kama hii, hasa kwa mama yangu si kijana na hawezi kusafiri mbali, kwa hiyo ninatakiwa kumfurahisha. Baba atahudhuria mechi ya fainali." 

Balotelli, kwa mabao hayo mawili aliyofunga, yamemwezesha kuwa miongoni mwa wachezaji wanaoongoza kwa kufunga mabao mengi kwenye michuano hiyo, akiwa amekwamisha wavuni mabao matatu. "Nitajaribu kufunga ili nitwae kiatu cha dhahabu," alisema. 

Alishangilia bao la pili kwa mtindo wa aina yake, kwa kuvua fulana na kusimama kimya. "Sikuchukia kwa sababu nilioneshwa kadi ya njano, lakini waliona ukakamavu wangu," alitania. 

Balotelli, ambaye alipumzisha kipindi cha pili, alimaliza utata kuwa, atakuwemo katika kikosi kitakachocheza kesho mechi ya fainali .

No comments