Header Ads

ad

Breaking News

Juventus yamfuatilia Balotelli Euro 2012


Balotelli
ROMA, Italia
WAKURUGENZI wawili wa klabu ya Juventus,  Fabio Paratici na Beppe Marotta, wamekwenda nchini Poland kufuatilia kiwango cha mshambuliaji wa timu ya taifa ya Italia, Mario Balotelli. 

Corriere dello limeandika kuwa, Juve inavutiwa na mshambuliaji huyo wa Manchester City, na wakurugenzi wake wawili wamekwenda jijini Warsaw kuzungumza naye. 

Wakala wa Balotelli, Mino Raiola,  ana hofu kama Juve watakuwa na fedha za kuishawishi City kuwamchia mshambuliaji huyo. 

Mkurugenzi wa Juve, Pavel Nedved, wakati huo huo alisema: "Niliwasiliana na Zlatan Ibrahimovic kuhusu Balotelli. Aliniambia kuwa, Mario ni bora na alicheza naye."

No comments