Header Ads

ad

Breaking News

SERIKALI YAAMURU KUTUMIKA KWA MAFUTA YA NDEGE KUTOKANA NAUHABA WA MAFUTA YA TAA NCHINI



NA MWANDISHI WETU
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), imesema kutokana na uhaba wa mafuta ya taa uliyojitokeza nchini serikali ina mpango wa kuyatumia mafuta ya ndege kama mbadala wa mafuta hayo.
Akizungumza na Fullshangweblog jijini Dar es Salaam leo, Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa Mamlaka hiyo, Titus Kaguo alisema waliamua kuchukua hatua hiyo baada ya wafanyabiashara kuacha kuagiza mafuta hayo kwa muda mrefu sasa.
Alisema kitakachofanyika ni kubadili matumizi mafuta hayo ya ndege kwa kuyashusha daraja ili yaweze kutumika kama mafuta ya taa ambapo hayata kuwa na madhara kwa watumiaji.
“Wafanyabiashara hao waliacha kuagiza mafuta kutokana na baadhi yao, ambao si waaminifu kukosa nafasi ya uchakachuaji hivyo, kupunguza kasi ya uingizaji wa mafuta hayo”alisema Kaguo
Kaguo alisema wafanyabiashara hao walikuwa wakiingiza hadi lita milioni 30 kwa mwezi lakini baada ya serikali kufanikiwa kubana mianya ya  uchakachuaji kiwango cha uingizaji kimechuka hadi lita milioni 10 kwa mwezi.
Aidha, alisema licha ya mipango hiyo, bado  Mamlaka hiyo imefanya mawasiliano na kuiagiza Kampuni ya PIC kuagiza mafuta hayo katika kipindi muafaka ili kuwaondolea kero watumiaji wa mafuta hayo.
Kwa upande mwingine Kaguo alizungumzia juu ya magari yaliyokamatwa wakati yakisafirisha mafuta nchini Burundi kuwa wanaopaswa kujibu maswali hayo ni Mamlaka ya Mapato nchini (TRA).
Alitanabaisha kuwa mafuta yote yanayosafirishwa nje ya nchi yanasimamiwa na TRA hivyo yanapotokea matatizo wahusika wakwanza ni mamlaka hiyo.
Kaguo alisema hata hivyo, TRA iliwaomba ushirikiano ambapo walikubali na kwenda kuchukuwa sampuli na kuipeleka kwa mkemia mkuu ili kupata ufumbuzi.

No comments