Naibu Waziri ataka wanafunzi wazingatie michezo
Naibu Waziri, Kassim Majaliwa
WANAFUNZI nchini wametakiwa kuongeza juhudi katika michezo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kunufaika na sekta ya michezo katika ajira.
Wito huo ulitolewa juzi na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, Kassim Majaliwa, wakati alipokuwa akizindua mradi wa michezo kwa wote unaoendeshwa na Taasisi ya Michezo ya Amer kwa ufadhili wa nchi ya Finland.
Finland imekuwa ikitoa vifaa mbalimbali vya michezo kwa shule za msingi na sekondari mkoani Lindi.
Majaliwa amesema wakati umefika kwa wanafunzi kupenda michezo kwani licha ya kupata afya bora, pia ni ajira na kujenga mahusiano.
Majaliwa amewataka wazazi na walezi kuiunga mkono taasisi ya Amer ili iweze kufanikiwa katika malengo yao ya kuinua vipaji vya michezo kwa vijana.
Amewataka walimu wa michezo kutoa ushirikiano kwa wanafunzi wanaopenda michezo , kwa kuwafundisha kanuni na sheria.
Amesema iwapo walimu na wanafunzi watajizatiti kwenye michezo, wataweza kusaidia kupunguza utoro shuleni na kuongeza mahudhurio madarasani.
WANAFUNZI nchini wametakiwa kuongeza juhudi katika michezo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kunufaika na sekta ya michezo katika ajira.
Wito huo ulitolewa juzi na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, Kassim Majaliwa, wakati alipokuwa akizindua mradi wa michezo kwa wote unaoendeshwa na Taasisi ya Michezo ya Amer kwa ufadhili wa nchi ya Finland.
Finland imekuwa ikitoa vifaa mbalimbali vya michezo kwa shule za msingi na sekondari mkoani Lindi.
Majaliwa amesema wakati umefika kwa wanafunzi kupenda michezo kwani licha ya kupata afya bora, pia ni ajira na kujenga mahusiano.
Majaliwa amewataka wazazi na walezi kuiunga mkono taasisi ya Amer ili iweze kufanikiwa katika malengo yao ya kuinua vipaji vya michezo kwa vijana.
Amewataka walimu wa michezo kutoa ushirikiano kwa wanafunzi wanaopenda michezo , kwa kuwafundisha kanuni na sheria.
Amesema iwapo walimu na wanafunzi watajizatiti kwenye michezo, wataweza kusaidia kupunguza utoro shuleni na kuongeza mahudhurio madarasani.
No comments