MBUNGE COSATO CHUMI KKWA KUSHIRIKIANA NA WIZARA YA AFYA, WATOA MSADA WA GARI LA KUBEBA WAGONJWANE JIMBONI KWAKE
![]() |

MBUNGE wa Mafinga mjini, Mhe. Cosato Chumi kwa
kushirikiana na wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
wametoa msaada wa gari la kubeba wagonjwa (ambulance) kwa ajili ya matumizi ya
kituo cha afya cha Igohole, wilayani Mufindi, mkoani Iringa iliyopo katika
jimbo hilo.
Gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser lilikabidhiwa kwa
uongozi wa halmashauri ya mji wa Mafinga inayosimamia uendeshaji wa kituo hicho katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Igohole, mjini Mafinga.
uongozi wa halmashauri ya mji wa Mafinga inayosimamia uendeshaji wa kituo hicho katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Igohole, mjini Mafinga.
Akikabidhi msaada huo Mhe. Chumi alisema;
“napenda ifahamike kwamba gari hilo limenunuliwa na wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. uadilifu na uaminifu kwa serilikali ndio umetufanya tushirikiane vyema katika
mambo mengi kwa faida ya wananchi wa jimbo langu la Mafinga.”Alisema.
“napenda ifahamike kwamba gari hilo limenunuliwa na wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. uadilifu na uaminifu kwa serilikali ndio umetufanya tushirikiane vyema katika
mambo mengi kwa faida ya wananchi wa jimbo langu la Mafinga.”Alisema.
Alisema gari hilo la wagonjwa ni rafiki kwa wagonjwa na wajawazito
kwa kuwa lina vifaa tiba vinavyoweza kutumika kutolea huduma wakati mgonjwa
akipelekwa hospitalini.
Baada ya kukabidhi gari hilo, Mhe. Chumi ambaye ni mbunge wa kwanza wa
jimbo hilo jipya, mkoani Iringa alikumbusha vipaumbele vyake kwa wapiga kura
wake kuwa ni kuhakikisha jimbo la mafinga
mjini linapata huduma bora ya maji, elimu, afya na miundombinu ya barabara.
mjini linapata huduma bora ya maji, elimu, afya na miundombinu ya barabara.


Baadhi ya wananchi waliojitokeza
wakati wa kupokea msaada wa gari hilo la kubebea wagonjwa lilotelewa na mbunge
wa Mafinga Mjini, Mhe. Cosato
Chumi kwa kushirikiana na wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto (Habari, Picha na Fedy Mgunda)
No comments