TAKUKURU YAWABURUZA MAHAKAMANI WALIMU WAWILI NA WALIOKUWA WATUMISHI HAI
Joyce Anael, Hai
engine
waliounganishwa katika kesi hiyo ni Alizan Abdallah Mruma ambaye ni
mwalimu wa shule ya sekondari Rau iliyoko manispaa ya Moshi na Athman
Abdul Mbowe mwalimu wa Shule ya sekondari Udoro iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Hai.
Washtakiwa
hao kwa pamoja wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na makosa ya kula
Njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za udanganyifu na kujipatia kiasi
cha fedha cha shilingi Milion Thelathini na Tano (35,000,000)kwa njia ya
udanganyifu kutoka Benki ya CRDB Tawi la Hai.
Mwendesha mashtaka wa Takukuru, Barry Galinoma aliwafikisha watuhumiwa hao mahakamani juzi mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya Wilaya ya Hai Mheshimiwa Anord Kyirakyando.
Katika
kesi hiyo ya Jinai Namba ECC.11/2017,mwendesha Mashtaka wa Takukuru
alidai kuwa washtakiwa hao kwa pamoja, walikula njama na kutengeneza
vitambulisho kwa kutumia majina ya watumishi waliostaafu katika
Halmashauri ya Wilaya ya Hai na kisha wakabandika picha za Alzan Abdalla
Mnduma na Athuman Abdul Mbowe kwenye vitambulisho hivyo.
Baada
ya kutengeneza vitambulisho hivyo mshtakiwa Faraja na Bayege, waliandaa
Check Namba za udanganyifu na kasha kufanya udhamini kwa Alizan na
Athuman katika Benki ya CRDB na kuonyesha kuwa watajwa kwenye
vitambulisho hivyo vya kughushi ni watumishi wa Halmashauri na kushauri
wapewe mkopo na Benki.
Imedaiwa
mahakamani hapo washakiwa hao walitenda kosa hilo kati ya Januari 2014
na octoba 31,2015 katika Halmashauri ya Wilaya ya Hai na kutokana na
udanganyifu huo washtakiwa hao waliweza kujipatia kiasi cha sh. milioni
35.
Hata
hivyo washtakiwa Alizan Mruma na Thuman Mbowe wamekana mashtaka hayo na
kwamba Mbowe yuko nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya Dhamana
huku mshtakiwa Alizan Mruma akipelekwa mahabusu baada ya kushindwa
kutimiza masharti ya Dhamana.
Washtakiwa
Faraja Ndatu na Isaiah Bayege, hawakuwepo mahakamani hapo wakati
mashtaka hayo yakisomwa ambapo mahakama ilitoa hati ya wito ili waweze
kufika mahakamani hapo kusomewa mashtaka yanayowakabili, na kwamba kesi
hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Oktoba 3, 2017.
No comments