OJ Simpson. (Getty Images)
Mchezaji nyota wa
soka la Marekani a pia muigizaji OJ Simpson amesamehewa kifungo chake
cha miaka 33, miaka 9 tu baada ya kuingizwa katika Gereza la Nevada.
Simpson anatumikia kifungo kutokana na kosa la uvamizi wa kutumia silaha nzito pamoja na makosa mengine 10 aliyoyafanya mwaka 2007 alipovamia Hotel mjini Las Vegas.
Alikuwa pia ameachiwa mwaka 1995 alipokuwa anakabiliwa na kesi ya mauaji ya mkewe.
Mwaka 2008, miaka 13 kamili baada ya kuondolewa mashitaka ya iliyoitwa 'Kesi ya karne' alikutwa na hatia ya uvamizi wa hotel.
Yeye pamoja na kundi la watu wengine watano walivamia Hotel na kuelekea katika eneo linalotunza vifaa vya michezo, wakakwapua vitu ambavyo alidai vilikuwa vyake kutokana na ushiriki wake michezoni.
Katika harakati za masamaha huu, OJ Simpson aliwaambia maafisa wa jopo la msamaha kuwa vitu alivyovichukua katika uvamizi ule hata hivyo vilikuja kugundulika kuwa vilikuwa vyake.
"Nimeishi maisha yasiyo ya mgogoro" alisema katika kikao kilichodumu kwa saa moja.
OJ Simpson alipata umaarufu mkubwa duniani kutokana na kesi iliyokuwa inamkabili ambapo ilidaiwa alimuua aliyekuwa mkewe pamoja na rafiki yake.
No comments:
Post a Comment