Header Ads

ad

Breaking News

Yanga yatupwa nje SportPesa Super Cup, fainali kuwakutanisha Wakenya

Beki wa Yanga, Juma Abdul, (kulia) akiruka kuwania mpira na beki wa AFC Leopards Abwao Marcus, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, jana Juni 8, 2017. Picha zote kwa hisani ya Montage Ltd
 

MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Yanga, leo imeaga michuano ya SportsPesa Super Cup, kwa mikwaju ya penalty baada ya kutoka suluhu katika muda wa kawaida wa dakika 90, kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Kwa matokeo hayo, Yanga wanaungana na watani wao wa jadi Simba, walioondoshwa na Nakuru All Stars, pia kwa njia hiyo hiyo ya mikwaju ya penalti.


Yanga imeondoshwa kwa penalty 4-2 dhidi ya mabingwa wa Kenya, AFC Leopards, huku wachezaji Said Mussa na Said Makapu wakishindwa kukwamisha wavuni mipira yao, lakini nahodha wa timu hiyo, nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Obrey Chirwa, wakizitikisa nyavu za wapinzani wao.

Kwa ushindi huo wa Leopards, ni dhahiri fainali itawakutanisha wakenya, hivyo timu mojawapo kupata nafasi ya kucheza na Everton ya England inayoshiriki Ligi Kuu.




Mshambuliaji wa Yanga Obrey Chirwa, akijiandaa kupiga shuti huku akizongwa na mabeki wa AFC Leopards, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, jana Juni 8, 2017

Mshambuliaji wa Yanga Juma Mahadhi (kulia) akimtoka mpira na beki wa AFC Leopards, Abdallah Salim, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, jana Juni 8, 2017.
Winga wa Yanga, Yusuph Mhilu (kushoto) akimfinya beki wa AFC Leopards, Abwao Marcus, wakati wa mchezo Nusu Fainali wa mashindano ya SportPesa Super Cup, uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, jana Juni 8, 2017

No comments