Header Ads

ad

Breaking News

KULIOMBEA TAIFA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU YA KAMILIKA LITAFANYIKA UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM, OKTOBA 4, 2015



 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Msama Promotion ambayo inaandaa matamasha mbalimbali kama lile la Pasaka  na Chrismas , ambaye ni Mwenyekiti wa Tamasha hilo, Alex Msama, akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya Tamasha la kuliombea Taifa Amani kuelekea uchaguzi mkuu ambalo litafanyika Oktoba 4, 2015 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na baadaye mikoa mingine 12.
 Hapa mkutano na wanahabari ukiendelea.
Wanahabari wakisubiri kuchukua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale

Mwimbaji wa kimataifa wa nyimbo za injili kutoka nchini Afrika Kusini, Solly Mahlangu, amethibitisha 
kutumbuiza katika tamasha la kuombe amani  linalotarajiwa kufanyika Oktoba 4 katika uwanja wa Taifa 
jiji Dar es Salaam.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Msama Promotion ambayo inayoandaa matamasha mbalimbali kama lile la Pasaka  na Chrismas , ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tamasha hilo kutoka kampuni hiyo, Alex Msama wakati akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu kukamilika kwa  maandalizi ya tamasha hilo sambamba na kutaja majina ya waimbaji wa nyimbo za injili wa ndani na nje ya nchi, wanaotarajiwa kutumbuiza katika tamasha hilo linalolenga kuombea nchi amani  hususani uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba 25 mwaka huu.

No comments