Saturday, February 23, 2013

Wenger kusajili mashine kali Julai

Arsenal Wenger
LONDON, England
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenge, amesisitiza kuwa, hayupo mbali na changamoto za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Englanda na Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Katika taarifa yake, kocha huyo alisema kwamba,  baada ya wiki ya kipigo katika mechi ya Kombe la FA dhidi ya Blackburn, kabla ya kuchapwa mabao 3-1 dhidi ya Bayern Munich kwenye uwanja wake wa Emirates, aliweka wazi kuwa, kikosi cha Gunners kiko ukingoni kumaliza ukame wa makombe wa miaka nane.
Hata hivyo, kocha huyo wa Arsenal, alisisitiza kuwa, ataongeza wachezaji wakali wanaohitajika katika kikosi chake ambacho kitakuwa cha ushindani chenye mshikamano.
"Hatuko mbali sana, hata kama ni vigumu kukushawishi leo," alisema Wenger. "Tuna msingi wa timu ambao ni imara, tunatakiwa kukiimarisha kikosi kwa kuangalia nafasi za kuzijaza zilizoonesha udhaifu.
"Hatuna tofauti kubwa na timu kama Bayern, walio katika nafasi kama ilivyo kwa Manchester United. Wanaweza kumudu kile wanachotaka kukifanya. Wako vizuri kiuchumi. Ukizipeleka Chelsea na Man City Ujerumani, utasikia tena kuhusu Bayern.
Wenger aliwataka mashabiki wa Arsenal kuwa wavumilifu, huku akithibitisha kuwa, anauamini uwezo wake na kikosi chao kitarajea katika makali yao.

No comments:

Post a Comment