MSHAMBULIAJI wa zamani wa Chelsea, Didier
Drogba, amewakumbusha Chelsea, makali yake baada ya kupiga bao katikam mechi
yake ya kwanza akiwa amevaa uzi wa Galatasaray, jana.
Mchezaji
huyo kutoka Ivory Coast, alifunga bao hilo katika mechi ambayo waliibuka na
ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Akhisar Belediyespor, likiwa bao lake la kwanza
barani Ulaya tangu alipofanya hivyo, katika mechi ya fainali ya Ligi ya Klabu
Bingwa Ulaya mwaka jana.
Kwa
mtindo wake uliozoeleka, Drogba alirukja juu na kuifungia Galatasaray bao hilo
dakika ya 68.
Mshambuliaji huyo alitoa mchango mkubwa
kwa Chelsea msimu uliopita na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la FA na Klabu
Bingwa Ulaya mwaka 2012.
Drogba aliitumikia Chelsea kwa muda wa miaka
nane na kuihama msimu uliopita, baada ya kushindwa kuongezwa mkataba aliokuwa
akiutaka.
Uamuzi wa mshambuliaji wa Atletical
Madrid, Radamel Falcao’, kuamua kubaki
katika klabu yake, umekuwa mzuri, huku Fernando Torres, akipigania kurejesha
makali yake aliyokuwa nayo wakati akiitumikia Liverpool.
Mashabiki wa Chelsea wanaona bora
mshambuliaji wao wa zamani, Drogba, angeendelea
kubaki katika klabu hiyo na kuwapa raha.
No comments:
Post a Comment