Sunday, February 17, 2013

Chelsea yaibuka na ushindi FA Cup

Frank Lampard (kushoto) na John Terry
LONDON, England
Chelsea, jana iliibuka na ushindi wa mabao 4-0, katika mechi ya kuwania kombe la FA raundi ya tano iliyochezwa kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, jijini London.
Juan Mata aliifungia Chelsea bao la kwanza dakika ya 54, baada ya kipindi cha kwanza kumalizika wakiwa hawajafungana.
Chelsea walijipatia bao la pili dakika ya 68, kupitia kwa  Oscar baada ya kupiga shuti kali lililomgonga Simon Moore na kujaa wavuni.
Frank Lampard, ambaye ataweza kuondoka katika timu hiyo, aliifungia bao la tatu Chelsea, akitumia vizuri mpira wa krosi uliopigwa na Oscar na kujaa wavuni.
Beki aliyekuwa majeruhi kwa muda mrefu, John Terry, aliifungia timu yake bao la nne kwa kichwa, akitumia vizuri mpira wa krosi wa  Oscar.

No comments:

Post a Comment