Header Ads

ad

Breaking News

Waziri Kawambwa amwaga vifaa Bagamoyo


Waziri Shukuru Kawambwa

WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Bagamoyo, Dk Shukuru Kawambwa, ametoa vifaa mbalimbali vya michezo kwa madiwani wa jimbo la hilo.
Kawambwa ametoa vifaa hivyo ikiwa ni moja ya njia za kuhamasisha ushiriki wa timu katika michuano ya kombe la madiwani hao katika kata saba za jimbo hilo.
Akizungumza katika hafla fupi ya kuwakabidhi vifaa hivyo, Dk Kawambwa alisema kuwa, ameamua kutoa msaada huo wa vifaa kwa lengo la kuwasaidia madiwani hao ili waweze kuendesha michuano kwa timu kutoka katika kata zao.
Alisema vifaa hivyo vitazisaidia timu zao ambazo ndio washiriki wa michuano ya Kombe la Kawambwa ambayo hufanyika kila mwaka wilayani humo.
“Kwa ujumla napenda kuwashurukuru madiwani hawa kwanza kwa kuniunga mkono katika michuano iliyopita lakini kubwa zaidi kazi nzuri waliyoifanya kwa ushirikiano mkubwa na kamati yangu ya jimbo.
“Kwa jumla ya miaka yote saba mbapo michuano hii imechezwa madiwani mmeweza kusimamia vizuri na kuleta changamoto kubwa katika michezo,” alisema Kawambwa
Akizungumzia mafanikio ya michuano hiyo, Kawambwa alisema kuwa michuano hiyo ya madiwani na hatimaye “Kawambwa Cup” imekuwa na mafanikio makubwa kwa vijana wilayani Bagamoyo kwani wengi wao wameweza kupata nafasi za masomo na wengine kusajiliwa na timu kutoka mikoa mingine nchini.
Alisema kuwa lengo kubwa la kuwapo kwa mashindano kama hayo ni kutaka kuwahamasisha vijana kuona kuwa michezo inaweza kutumika kama ajira mbadala hata kwa vijana ambao hawana elimu kutokana na matatizo mbalimbali.
Alisema kuwa michuano ya Kawambwa Cup mwaka huu inatarajiwa kugharimu Sh. milioni 28, tofauti na ile ya mwaka jana ambayo ilitumia Sh. Milioni 26 na imekuwa ikidhamini kwa ushirikiano mkubwa baina ya ofisi yake na kampuni ya Tanzania Distrlies Limited watengenezaji wa Konyagi.

No comments