Simba, Azam fainali ya Ujirani Uwanja wa Taifa kesho
![]() |
Simba SC |
MABINGWA wa
soka wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba,
na mabingwa wa Kombe la Mapinduzi Zanzibar, Azam FC, kesho zitashuka Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam, kuumana katika mechi ya fainali ya Kombe la Ujirani
Mwema.
Awali,
michuano hiyo ilikuwa ikichezwa kisiwani Zanzibar, lakini hatua ya fainali
imehamishiwa jijini Dar es Salaam.
Uamuzi huo
umefikiwa jana baada ya timu hizo mbili kujadiliana na uongozi wa Chama cha Soka
Zanzibar (ZFA) na kuamua kuihamishia Uwanja
wa Taifa jijini Dar es Salaam na kuisongeza mbele siku moja.
Habari kutoka
ndani ya kikao hicho zilisema kwamba, Simba na Azam ziligoma kuendelea kuutumia
Uwanja wa Amani mjini humo, kwa madai kuwa, ni mbovu.
“Timu hizi
zilikuwa zikitumia uwanja huu huku zikilalamika kuwa, ni mbovu na wachezaji wao
wameumia,” kilisema chanzo hicho.
Habari zaidi
zilisema kuwa, Simba na Azam, zote zina wachezaji watatu waliokuwa majeruhi,
ambao waliumia wakati wakizichezea timu zao kwenye Uwanja huo wa Amani.
Kutokana na
ubovu huo, viongozi wa timu hizo ambazo zitashiriki michuano ya Klabu Bingwa
Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), waliamua kuhamishia mechi hizo
kwenye uwanja ambao utawafanya wachezaji wao wachezaji bila ya hofu.
Chanzo hicho
kiliongeza kwamba, Kampuni ya Prime Time Promotion, ndio waliochukua pambano
hilo na watatoa sh. milioni 25 kwa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), mshindi sh.
milioni 10 na wa p[ili sh. milioni tano.
Awali,
fainali hiyo ilikuwa ichezwe leo kwenye Uwanja wa Amani Zanzibar, lakini baada
ya kuihamishia jijini Dar es Salaam, wameamua kusogeza mbele siku moja.
Mara ya mwisho
timu hizo zilikutana katika hatua ya makundi na kutoka sare ya bao 1-1, mabao
hayo yalifungwa na wachezaji wapya wa timu hizo waliosajiliwa kwa ajili ya msimu
ujao wa Ligi Kuu, Dany Mrwanda kwa upande wa Simba na Azam FC ikasawazaisha
kupitia kwa George Odhiambo ‘Blackberry’.
Pamoja na kutoka
sare katika mchezo huo, Azam FC walicheza pungufu baada ya kiungo wake, Abdulhalim
Humoud, kutolewa nje kwa kadi kuoneshwa kadi nyekundu dakika ya 52, baada ya kuoneshwa kadi ya njano mara mbili
kwa kucheza vibaya.
Mchezo huo
unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimuwa, kutokana na timu hizo kuwa na upinzani
wa hali ya juu, huku kila moja iktumia wachezaji wapya waliosajiliwa kwa ajili
ya ligi ya Bara msimu ujao.
![]() |
Azam FC |
No comments