TASWA WAMLILIA PATRICK MUTESA MAFISANGO
![]() |
Wachezaji wa timu ya taifa wakiwa wamebeba jeneza la lililokuwa na mwili wa Mafisango |
CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA),
kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha kiungo wa timu ya
Simba ya Dar es Salaam na mchezaji wa timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi),
Patrick Mutesa Mafisango kilichotokea alfajiri ya Alhamisi kwa ajali
ya gari jijini Dar es Salaam.
Katibu wa TASWA,
Amir Mhando ameiambia BIN ZUBEIRY mchana huu kwamba, wanatoa pole kwa
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage, wachezaji wa timu hiyo, mashabiki na
Watanzania kwa ujumla kutokana na msiba huo mkubwa kwa familia ya mpira
wa miguu.
"Tunaamini
waandishi wa habari za michezo wameguswa kwa kiasi kikubwa na msiba
huo, kwani wakati wa uhai wake marehemu alikuwa na ushirikiano mkubwa na
wanahabari na hakuwa mtu mwenye maringo, kiasi cha kushindwa kutoa
ushirikiano kwa wenzake,"alisema.
Alisema
kifo chake ni pigo si kwa Simba na familia yake tu, bali hata kwa timu
ya Taifa ya Rwanda na Wanyarwanda wote, ambao pia tunawapa pole kwa
msiba huo.
"Tunawapa
pole wanamichezo wote na kuwaomba wawe na subira na uvumilivu katika
kipindi hiki kigumu, huku wakiamini waandishi wa habari za michezo tupo
nao pamoja katika majonzi hayo na kumuomba Mungu aiweke roho ya marehemu
mahali pema peoni. Amina,"alisema Mhando.
Wakati
huo huo: Mhando amesema kuwa mtangazaji wa habari za michezo wa Redio
Uhuru, Limonga Justine, amefiwa na baba yake mzazi jana Alhamisi asubuhi
kwenye hospitali ya Temeke, Dar es Salaam. alisema
msiba upo Mbagala kwa Mangaya, Dar es Salaam na maziko yanatarajiwa
kufanyika kesho Jumamosi. Naomba tuungane naye mwenzetu katika kipindi
hiki kigumu kwake na tumfariji kwa kadri tuwezavyo kwa kuondokewa na
mzazi wake.
No comments