Header Ads

ad

Breaking News

7,186 WASHUHUDIA MECHI YA TOTO AFRICANS, YANGA


Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Toto Africans na Yanga iliyochezwa juzi (Aprili 15 mwaka huu) kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ilishuhudiwa na watazamaji 7,186 na kuingiza sh. 15,392,000. Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000 kwa jukwaa kuu na sh. 2,000 mzunguko.
 
Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 2,347,932 kila klabu ilipata sh. 2,729,060, uwanja sh. 909,686.
 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 909,686, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) sh. 363,874, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 454,843, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh. 90,968 na asilimia 10 ya gharama za mechi ni sh. 909,686.
 
Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya ndani kwa waamuzi sh. 10,000, nauli ya ndani kwa kamishna wa mchezo sh. 10,000. Mwamuzi wa akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa kamishna na waamuzi sh. 160,000, gharama ya tiketi sh. 2,300,000.
 
Gharama nyingine ni Jichangie ambayo ni sh. 200 kwa kila tiketi; kila klabu ilipata sh. 503,020 wakati Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) kilipata sh. 431,160.
 

No comments