Friday, May 18, 2012

Makocha 24 waomba kazi Yanga


JUMLA ya makocha 24 kutoka nchi mbalimbali, wamejitokeza kuomba kazi ya kufundisha klabu ya Yanga ya Dar es Salaam, nafasi iliyoachwa wazi na Mserbia Kostadin Bozidar Papic.
Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu amaeiambia BIN ZUBEIRY mchana huu kwamba, makocha waliojitokeza ni kutoka Uholanzi, Scotland, Serbia na Ujerumani .
 
Sendeu alisema wengine wanatokea England  na Ureno anakotokea Cristiano Ronaldo.
 
Sendeu alisema Kamati ya Ufundi bado inapitia wasifu wa makocha hao kabla ya kupendekeza watatu wa kuingia kwenye mchujo wa mwisho, ambao miongoni mwao atapatikana kocha mpya wa Yanga.
 
Aidha, Sendeu alisema kwamba Kamati ya Utendaji ya Klabu ya Yanga, imeahairisha Mkutano wake na Wazee, ili kushughulikia mambo mengine yaliyojitokeza ikiwa ni pamoja na mapendekezo ya Yussuf Manji.

No comments:

Post a Comment