Tuesday, May 22, 2012

Abdial wa Barcelona atoka hospitali


Abidal

BARCELONA, Hispania
BEKI wa klabu ya Barcelona, Eric Abidal, ameruhusiwa kutoka hospitali baada ya kufanyiwa matibabu ya ini mwezi.

Abidal mwenye miaka 32, alithibitisha kuhitaji kufanyia matatibu ya kupandikizwa ini mapema mwaka huu, yapata mwaka baada ya kutakiwa kufanyiwa upasuaji wa ini. 

Taarifa fupi ya Barcelona ilisema: "Beki huyo mfaransa alitolewa hospitali jana baada ya kupandikizwa ini Aprili 10, mwaka huu. 

"Daktari wa timu alieleza kuwa,: 'Nilipewa taarifa za maendeleo yake yanavyokwenda. Abidal ataendelea kuripoti hospitali kwa uchunguzi mara kwa mara.'"

Kufuatia upasuaji wake wa kwanza Machi 2011, Abidal alikuwa nje kwa muda wa wiki saba, alirejea mwishoni na kucheza baadhi ya mechi akitokea kwenye benchi.

No comments:

Post a Comment