SERIKALI YAAINISHA MKAKATI WA KUWAELEZA WANANCHI UTEKELEZAJI WA AHADI ZAKE
Mkurugenzi wa Idara
ya Habari (MAELEZO) ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Hassan Abbasi
akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam leo kueleza mikakati ya
kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi kupitia utoaji wa taarifa kwenye
vyombo mbalimbali vya habari kuhusu utekelezaji wa ahadi za Serikali ya Awamu
ya Tano. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara hiyo upande wa Habari Bw.
Vincent Artemony Tiganya.
Waandishi wa Habari
kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakifuatilia ufafanuzi uliokuwa ukitolewa
na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa
Serikali Hassan Abbasi, juu ya mikakati ya Serikali katika kuimarisha mawasiliano
kati ya Serikali na wananchi kupitia utoaji wa taarifa mbalimbali za utekelezaji
wa ahadi za Serikali ya Awamu ya Tano
Mkurugenzi wa Idara
ya Habari (MAELEZO) ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Hassan Abbasi
akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam leo kueleza mikakati ya
kuimarisha mawasiliano kati ya Serikali na wananchi kupitia utoaji wa taarifa kwenye
vyombo mbalimbali vya habari kuhusu utekelezaji wa ahadi za Serikali ya Awamu
ya Tano.Picha/ Aron Msigwa
Na. Immaculate
Makilika - Dar es salaam.
Serikali imesema kuwa itaanza
kutekeleza mikakati mbalimbali inayoloenga kuwapatia wananchi taarifa za kila
mara kuhusu utekelezaji wa ahadi zake
Akizungumza na waandishi wa
habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO Bw.
Hassan Abbasi alisema kuwa Serikali imeandaa mikakati ambayo itasaidia kuongeza
uwazi na ushirikishaji ili kuwawezesha wananchi kupata mbalimbali taarifa kwa
wakati.
“ Mawaziri wote wataanza
kuonekana kwenye vyombo vya habari kuanzia wiki ijayo wakielezea vipaumbele na kuainisha mafanikio na
changamoto za utekelezaji wa mipamgo na sera mbalimbali na hili ni zoezi endelevu” alisema Bw. Abbasi.
Aliongeza kuwa, lengo ni kutoa
taarifa ya utekelezaji kwa wananchi kuhusu mipango mbalimbali ya Serikali
kupitia wizara ambapo wataelezwa kuhusu vipaumbele vya wizara na nini
kinafanyika.
Bw. Abbasi, ametaja mikakati hiyo
kuwa ni kuboresha mfumo wa Mawaziri na Watendaji waandamizi wa serikali
kuzungumza na wananchi ili kuanisha
utekelezaji wa vipaumbele vya bajeti,
sera na mipango ya Taifa inayosimamiwa
na Wizara husika.
Aidha, mkakati mwingine ni
kuanzisha utaratibu wa Idara ya Habari- MAELEZO kueleza kwa umma kila mara kuhusu
utekelezaji wa sekta zote katika ngazi ya kitaifa ambapo hivi karibuni Msemaji wa serikali atakuwa akitoa taarifa hizo.
Akizungumzia kuhusu mpango wa
kuimarisha mahusiano na wadau mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari, Abbasi
alisema kuwa Idara ya Habari -MAELEZO imejipanga kufanya kazi kwa karibu ili
kuhakikisha kwa pamoja wanaleta mapinduzi
katika sekta ya Mawasiliano nchini.
Mawaziri wanatarajiwa kutoa
taarifa kwa umma kupitia vyombo mbalimbali vya habari kuanzia Agosti 25 mwaka
huu.
No comments