Mikataba ya madini, gesi, mafuta kupitiwa na timu ya wataalam kabla ya kusainiwa
Mtaalam kutoka Kitengo cha Nishati na Mabadiliko ya Tabia Nchi, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Abbas Kitogo akielezea mkakati wa shirika la UNDP katika kuwajengea uwezo wataalam kutoka taasisi za Serikali kuhusu usimamizi wa mikataba kuhusu madini, gesi na mafuta katika warsha hiyo.
Washiriki wa warsha kuhusu Dira ya Madini Afrika wakifuatilia kwa makini hotuba ya ufunguzi iliyokuwa inatolewa na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (hayupo pichani).
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (watatu kushoto waliokaa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo kuhusu Dira ya Madini Afrika iliyofanyika mjini Morogoro tarehe 21 Septemba, 2015.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (kulia) akifungua warsha kuhusu Dira ya Madini Afrika iliyokutanisha wataalam kutoka taasisi za serikali nchini lengo likiwa ni kuwapa uelewa juu ya sekta ya madini na usimamizi wa mikataba.
Kaimu Mkurugenzi wa Mikataba kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Evelyne Makala akisisitiza jambo kwenye mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
Sektretarieti ikifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa kwa nyakati tofauti.
Mratibu
wa Mradi wa Biofueli, Wizara ya Nishati na Madini, Paul Kiwele, ( wa
kwanza kushoto mbele) Kamishna Msaidizi wa Madini- Uchenjuaji na
Uongezaji Thamani Madini, Mwacha Mtoro ( wa pili kutoka kushoto,
mbele) pamoja na washiriki wengine wakifuatilia kwa makini mada
mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa.
Greyson Mwase, Morogoro
ILI kuhakikisha kuwa wananchi wa Tanzania
wananufaika na rasilimali
za madini mbalimbali pamoja
na gesi iliyogunduliwa kwa wingi hivi
karibuni, Serikali imeanza kutoa mafunzo kwa wataalam kutoka taasisi za
serikali watakaohusika na upitiaji wa
mikataba yote ya shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini, gesi na mafuta kabla ya kusainiwa.
Hayo
yalisemwa na Waziri wa Nishati na
Madini, George Simbachawene katika uzinduzi wa warsha kuhusu dira
mpya ya madini Afrika
iliyofanyika mjini Morogoro.
Warsha
hiyo ya siku tatu iliyoandaliwa na Wizara ya Nishati na Madini
ilikutanisha wataalam kutoka taasisi za serikali ikiwa ni pamoja na Ofisi
ya Makamu wa Rais, Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha,
Ofisi ya Rais- Tume ya Mipango, Mamlaka
ya Mapato Nchini (TRA) na Taasisi ya
Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF).
Pia ilikutanisha wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini pamoja na taasisi zake
kama vile Wakala wa Ukaguzi wa
Madini Nchini (TMAA), Shirika la Madini
la Taifa (STAMICO), Shirika la Uendelezaji Nishati ya Jotoardhi
Tanzania (TGDC), Mpango wa Kuongeza Uwazi na Uwajibikaji katika Tasnia ya
Uziduaji Nchini (TEITI), Mamlaka ya
Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji
(EWURA) na Chuo cha Madini Dodoma (MRI).
Simbachawene
alisema uundaji wa timu ya wataalam mbalimbali kwa ajili ya kupitia mikataba ya
madini, gesi na mafuta ni moja ya
makubaliano katika utekelezaji wa Dira ya Madini ya
Africa (Mining Vision for
Africa) iliyoasisiwa na wakuu wa
nchi zenye madini katika mkutano wake uliofanyika mwaka 2009.
Alisema
kuwa katika kuhakikisha kuwa sekta ya madini inachangia katika ukuaji wa uchumi
wa nchi za Afrika zinazozalisha madini
wakuu wa nchi walikubaliana kuanzishwa kwa Dira ya Madini itakayowezesha sekta ya madini katika nchi wanachama
kuboreshwa na kuwa na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi.
Alisema
kuwa katika utekelezaji wa Dira ya Madini ya Afrika, nchi ya
Tanzania imeanza kutoa mafunzo kwa wataalam mbalimbali katika taasisi za Serikali katika upitiaji wa mikataba hususan ya
utafiti na uchimbaji wa rasilimali za madini, gesi na mafuta.
Alisisitiza
kuwa mara baada ya wataalam hao kupata mafunzo
wataweza kupitia mikataba mbalimbali kabla ya kusainiwa.
“Ieleweke
kwamba suala la mikataba litakuwa
si kati ya watu wawili bali wataalam
watashirikishwa kwa kupitia mikataba hiyo na kutoa mapendekezo yao kabla ya
mikataba kusainiwa na Waziri ambaye ni msimamizi wa sekta husika,” alisisitiza Simbachawene.
Akielezea
ushirikishwaji wa wananchi katika usimamizi wa
sekta za madini, gesi na mafuta, Simbachawene alisema kuwa Serikali
imehakikisha kuwa mikataba yote
inalenga kuwanufaisha wananchi kwa kushirikishwa katika utoaji wa huduma katika
sekta husika.
Akitolea
mfano wa sekta ya gesi nchini, alisema
fursa za utoaji wa huduma zipo nyingi na kuwataka wananchi kuchangamkia fursa hizo
Hata
hiyo alieleza kuwa Serikali ina mkakati
wa kutoa mafunzo kwa wanachi kuhusu uzalishaji wa bidhaa bora ili ziendane na
soko la kimataifa.
“Tunataka ifike mahali makampuni yanayofanya
shughuli za utafiti na uchimbaji wa madini, gesi na mafuta yanunue
huduma na bidhaa kwa wananchi wa
Tanzania badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi,” alisisitza Simbachawene.
Naye
mtaalam kutoka Kitengo cha Nishati na Mabadiliko ya Tabia Nchi, Shirika
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Abbas Kitogo alisema kuwa shirika la UNDP limekuwa likishirikiana na
Serikali katika utoaji wa mafunzo kuhusu sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja
na usimamizi wa mikataba.
Alisema
sekta nyeti kama za madini, gesi na mafuta zisiposimamiwa kikamilifu zinaweza
kuibua migogoro badala ya kuleta maendeleo.
Alisisitiza
kuwa kupitia mafunzo hayo wataalam kutoka
taasisi za serikali wataweza kupitia mikataba mbalimbali
ya utafiti na uchimbaji wa madini, gesi na mafuta na kuishauri serikali
kabla ya kusainiwa ili kutumika
rasmi.
No comments