POLISI WAUNDA TUME MAUAJI YA MWANDISHI WA HABARI
Askari
Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), wakimsulubu mtu anayedaiwa
kuwa Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel Ten Iringa, Daud Mwangosi
katika vurugu zilizotokea kati ya Polisi na wafuasi wa Chadema kwenye
Kijiji cha Nyololo, Mufindi. Katika vurugu hizo mwandishi huyo aliuawa
kwa kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu.
Polisi
wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) wakimsaidia mmoja wa askari
aliyeruhiwa katika tukio la kuuawa kwa mwandishi Daud Mwangosi huko
Nyololo, Mufindi mkoani Iringa
Mwili wa Daud Mwangosi baada ya kusambaratishwa na bomu. Aliyekaa jirani ni askari ambaye alijeruhiwa katika tukio hilo
Polisi wa FFU wakipiga mabomu ya machozi kutawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa katika ofisi za tawi la chama chao
Mkuu
wa Operesheni Sangara wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema
Benson Kigaila, akiwa katika gari la chama hicho pamoja na mmoja wa
majeruhi wa vurugu za polisi na wafuasi wa chama hicho
RPC katika maandalizi
Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wakipandishwa katika gari la Polisi
DAR ES SALAAM, Tanzania
JESHI la
Polisi nchini limeunda tume itakayochunguza kifo cha Mwandishi wa
Habari wa Kituo cha Channel Ten, Marehemu Daud Mwangosi kilichotokea
mjini Iringa wakati Jeshi la Polisi likipambana na wafuasi wa Chadema
waliokuwa katika ufunguzi wa tawi la chama hicho katika Kijiji cha
Nyololo mjini Iringa.
Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Polisi Paul Chagonja (pichani) amesema kuwa Uchunguzi
huo utavishirikisha vyombo vya usalama kutoka Jeshi la Polisi pamoja na
Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) "Jeshi la Polisi limeunda tume
itakayowahusisha Maofisa kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ
pamoja Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Robert Manumba, Inspekta Jenerali
wa Polisi (IGP), Said Mwema ili kubaini ukweli kuhusu kiliochosababisha
kifo cha mwandishi huyo basi tusubiri matokeo ya uchunguzi huo" alisema
Chagonja.
Marehemu
Mwangosi amefariki dunia jana wakati baada ya kulipukiwa na kitu
kinachachodaiwa kuwa ni bomu wakati chama cha Demokrasia na Maendelo
(Chadema) kikifungua tawi la chama vchake katika Kijiji cha Nyololo
mjini Iringa.
"Kwa sasa tayari Ispekta Generali wa Polisi (IGP), Said Mwema yupo mjini Iringa pamoja na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba pamoja na timu yake nzima kuanza rasmi kwa uchunguzi wa tukio hilo. Alisema Kamishna Chagonja".
"Kwa sasa tayari Ispekta Generali wa Polisi (IGP), Said Mwema yupo mjini Iringa pamoja na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba pamoja na timu yake nzima kuanza rasmi kwa uchunguzi wa tukio hilo. Alisema Kamishna Chagonja".
No comments