Header Ads

ad

Breaking News

Maximo: nitaijenga Yanga, kutua Jumanne


Marcio Maximo

KOCHA wa zamani wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’ aliyewezesha kupandisha soka nchini, Marcio Maximo, amesema kuwa, ataijenga vizuri Yanga na kuwa moja ya timu tishio barani Afrika.

Akizungumza kwa njia ya mtandao, Maximo alisema soka la Tanzania analifahamu, hivyo ana uhakika wa kukisuka vizuri kikosi hicho na kuleta ushindani mkubwa barani Afrika.

“Ninalijua soka la Tanzania, Afrika Mashariki na Afrika, nina uhakika wa kufanya mambo makubwa zaidi ya yale ya Stars,” alisema.

Kocha huyo aliwahi kuifikisha katika viwango vya soka duniani katika nafasi ya 100 bora na kuipa matumaini ya kuzidi kupanda kwa upamnde wa viwango.

Maximo, anatarajiwa kutua nchini Jumanne ijayo kwa ajili ya kuingia mkataba na klabu hiyo yenye maskani yake katika makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani jijini Dar es Salaam.

Taarifa zilizotua kwenye dawati la SuperStar zilisema kuwa,  baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, siku hiyo ya Jumanne ya Juni 12 mwaka huu, Maximo atakwenda moja kwa moja makao makuu ya klabu hiyo na kufanya mazungumzo ya faragha na uongozi wa Yanga. 

“Kocha akishawasili atakutana na uongozi kisha atawasaliamia wanachama na wapenzi wa Yanga na baadaye atakwenda kupunzika kisha kukutana naye kwa ajili ya kutia saini mkataba wa kuifundisha timu mbele ya wanahabari siku inayofuata.

“Baada  ya mambo hayo kukamilika tunarajia kikosi kitaitwa na kukunana na wachezaji wote waliosajiliwa kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, pamoja na michuano ya Kagame ambayo Yanga ni bingwa mtetezi.

“Pia kuna safari ya kwenda Unguja na Pemba kwa ajili ya kujiandaa na michuano hiyo ya Kagame, ambapo wanachana na wapenzi wa Yanga watakuwa na fursa ya kuiona wakati ikiwa katika harakati zake za kuutetea ubingwa wake,” kilisema chanzo chetu ndani ya Yanga.

Maximo, raia wa Brazil ni miongoni mwa makocha wenye uwezo mkubwa wa kushawishi mashabiki, kitu ambacho kinaweza kumsaidia kuungwa mkono katika majukumu yake.
Miongoni mwa majukumu atakayoanza nayo, ni kuhakikisha Yanga inalibakiza kombe la Kagame na kuutwaa ubingwa Bara msimu ujao.

Kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Taifa Stars, ndiye aliyekuwa chachu ya mashabiki kukishangilia kikosi cha Stars kinapokuwa na mechi.

No comments