Header Ads

ad

Breaking News

Maximo apewa jukumu Yanga


Maximo
 KOCHA wa zamani wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars, Mblazil Marcio Maximo, amepewa jukumu zito la kuwatafuta wachezaji wawili ili aje nao.

Maximo anatarajiwa kukinoa kikosi cha Yanga msimu ujao wa Ligi Kuu Bara, lakini kama tajiri wa klabu hiyo, Yusuf Manji, ataukwaa uenyekiti.

Manji alichukua fomu za kuwania uenyeji wa klabu hoyo, katika uchaguzi utakaofanyika Julai 15, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

 “Manji ana mipango mizuri ikiwa atashinda, kwanza anataka kumleta Maximo na kuwasajili wachezaji wawili kutoka Brazil,” alisema.

Tajiri huyo katika nafasi ya uenyekiti atakuwa akichuana na  John Jambele, Edger Chibura na Sarah Ramadhani.

Nafasi Makamu Mwenyekiti inawania na mchezaji wa zamani wa klabu hiyo, Ally Mayay, Ayoub Nyenzi, Yona Kevela na Clement Sanga.

Waanaowania ujumbe wa kamati ya utendaji ni Lameck Nyambaya, Ramadhani Mzimba ‘Kampira’, Mohamed Mbaraka, Ramadhani Said, Edgar Fongo, Beda Simba, Ahmad Gao, Mussa Katabaro, George Manyama na Aaron Nyanda.

Wengine ni Abdallah Bin Kleb, Omary Ndula, Shaaban Katwila, Jumanne Mohamed Mwammenywa, Abdallah Mbaraka, Peter Haule, Justin Baruti na Abdallah Sharia.

No comments