1,000/- TU KUONA TWIGA STARS, BANYANA BANYANA
![]() |
Boniface Wambura, Msemaji TFF |
Kiingilio
kwenye mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya timu ya Taifa ya wanawake
(Twiga Stars) na Afrika Kusini (Banyana Banyana) itakayochezwa Jumalipi
(Mei 20 mwaka huu) ni sh. 1,000.
Mechi
hiyo ambayo ni sehemu ya maandalizi kwa timu hizo zinazoshiriki
mashindano ya Afrika itafanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia
saa 10.30 jioni. Viingilio hivyo ni kwa maeneo yote, isipokuwa VIP A
ambapo itakuwa sh. 10,000 na VIP B sh. 5,000.
Baada
ya mechi hiyo, Twiga Stars itakwenda Ethiopia kwa ajili ya mechi ya
mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC)
itakayochezwa Mei 27 mwaka huu jijini Addis Ababa.
No comments